Katika ujumbe alioutuma kwenye mtandao wa kijamii wa X jana Ijumaa, Nasser Kan'ani ameeleza kuwa, "Ni kinaya chungu kwamba nchi hizo (za Magharibi) zinaikatia misaada UNRWA kwa kutegemea madai yasiyo na msingi yaliyotolewa na utawala ambao unatuhumiwa kufanya mauaji ya kimbari Gaza."
Kan'ani amebainisha kuwa, hakuna shaka kuwa hisia za kiutu zilizo na mwamko duniani zitahukumu uamuzi huo wa nchi za Magharibi wa kuwakatia misaada Wapalestina wakati huu ambao wanapitia mtihani na misukosuko.
Hivi karibuni, Ujerumani, Uswisi, Italia, Canada, Finland, Australia, Uingereza, Uholanzi, Marekani, Ufaransa, Austria na Japan zilitangaza kusitisha misaada yake kwa shirika la UNRWA kwa kutegemea madai ya Tel Aviv kwamba baadhi ya wafanyakazi wa shirika hilo wanaunga mkono oparesheni iliyotekelezwa na Harakati ya Hamas ya Kimbunga cha Al Aqsa mnamo Oktoba 7.
342/